Picha ya mwakilishi wa kina mama wa Migori aliyeponea ajali mbaya, hatimaye atabasamu

- Pamela Odhiambo alionekana kwa mara ya kwanza baada ya kuponea ajali mbaya iliyosababisha kifo cha mlinzi wake

- Katika picha hiyo, kiongozi huyo anaonekana akitabasamu japo kwa uchungu

- Mlinzi wake alifariki papo hapo katika ajali hiyo kwenye barabara kuu ya Rongo- Hoba Bay

Habari Nyingine : Mtoto wa nyoka ni nyoka; bintiye Akothee ajianika nusu uchi

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Picha ya mwakilishi wa kina mama katika kaunti ya Migori imeonekana kwa mara ya kwanza siku tano baada ya kuhusika katika ajali mbaya zaidi.

Habari Nyingine : Vijisababu 13 ambazo polisi hutumia kuwakamata watu kiholela usiku

Katika picha hiyo iliyoonwa na jarida la TUKO.co.ke, Pamela ambaye anaonekana kusisimka anatabasama huku amesimama kando ya kitanda chake hospitalini.

Kiongozi huyo alisafirishwa kutoka katika hospitali ya Agha Khan Kisumu hadi Nairobi kwa matibbau maalum baada ya kuponea kwa tundu la sindano katika ajali hiyo mbaya Jumapili, oktoba 8.

Habari Nyingine : Picha ya sosholaiti Mtanzania akipapasa sehemu nyeti ya mwanaume yazua hisia mseto

Wakati wa ajali hiyo, Pamela alikuwa njiani kujiunga na seneta wa Baringo Gideon Moi ambaye alikuwa katika kaunti hiyo kwa ziara maalum.

Kulingana na kiongozi wa polisi katika kaunti hiyo Joseph Nthenge aliyethibitisha kisa hicho, ajali hiyo ilitokea dereva alipojaribu kuhepa asimgonge mwendesha bodaboda kabla kupoteza udhibiti wa gari hilo.

Habari Nyingine : Vijisababu 13 ambazo polisi hutumia kuwakamata watu kiholela usiku

Kama ilivyoripotiwa awali na jarida la TUKO.co.ke, gari hilo lilibingiria mara kadhaa kabla kusimama.

Tofauti na Dennitah Ghati aliyekuwa seneta wa Migori aliyelazimika kutumia kiti cha magurudumu baada ya kuhusika katika ajali kama hiyo 2014, Pamela ataweza kutembea tena.

Ajali hiyo ilifanya katika barabara ya Ntulele, kaunti ya Narok, eneo linaloogopwa kwa visa vingi vya ajali.

Read ENGLISH VERSION

Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke ,kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdibn13gZdmp6KbmJZ6uq2Mpq6ao5mhtrS0yGaummWbnruiecyapJplp5Z6rrXGqKmiZZGhtrqxz6ilnpldlreiuMhmpJuZqZZ6qa3ToqSasZVirrWtwZqqmqWlY7W1ucs%3D