Jamaa aliyepasua mpira kitandani wakati wa mashambulizi atakiwa kuubeba msalaba wake

- Beta Healthcare imedai kuwa jamaa huyo alikuwa muongo na hawezi kuaminika

- Kampuni hiyo ya mipira ya kondomu ilimtaka jamaa huyo kuubeba msalaba wake kwa kuhusika kwa ngono nje ya ndoa

- Kulingana kampuni hiyo, jamaa huyo alikuwa amenunua kondomu isiyomtoshea

- Jamaa huyo alikuwa ameyashtaki mashirika ya KEBS na KRA kwa kuruhusu bidhaa feki kuuzwa sokoni

Habari Nyingine : Bosi wa benki maarufu aanikwa kwa kumpokonya gavana mke

Jamaa aliyeishtaki kampuni ya kutengeneza mpira wa kondomu Beta Healthcare baada ya kondomu yake kupasuka na kuambukizwa maradhi ya zinaa ataubeba msalaba wake mwenyewe.

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Kulingana na kampuni ya Beta Health Care, jamaa huyo alikuwa mwongo ambaye hangeweza kuaminika maana alikuwa amekiri kuwa alikuwa na uhusiano nje ya ndoa na huku ndiko mpira huo wa kandomu ulikopasukia.

Habari Nyingine : Binti mrembo ashangaza wengi baada ya kutangaza anaishi na virusi vya HIV

Kampuni hiyo iliiomba korti kufutilia mbali kesi hiyo ikidai kuwa hiyo ni kupoteza wakati na mali ya umma.

‘’ Mtu kama huyo atadanganya tena. Licha ya kueleza kuwa na mke, alikiri kuhusika katika ngono nje ya ndoa. Hii ni ishara kuwa yeye si mwaminifu na hawezi kuaminika,’’ kampuni hiyo iliandika..

Habari Nyingine : Huyu ndiye mwanamke anayelipwa mshahara mkubwa zaidi ulimwenguni?

Kampuni hiyo ilidai kuwa jamaa huyo alichora taswira ya mtu mdanganyifu maana alikiri kuwa na uhusiano nje ya ndoa licha ya kuwa na mke.

Wakijitetea, kampuni ya Zoom ambayo ndiyo kampuni ya kondomu hiyo ilimtaka kutoa thibitisho kuwa aliinunua kondomu ‘size yake’.

Habari Nyingine : Binti mrembo ashangaza wengi baada ya kutangaza anaishi na virusi vya HIV

‘’ Iwapo mlalamishi alinunua kondomu ya Zoo, ni vyema aseme kama alinunua inayomtoshea. Hiyo ndiyo sababu ilipasuka, madai ambayo hajayathibitisha,''

Jamaa huyo aliishtaki kampuni hiyo akidai kuwa alitumia kondomu yao kwa mpango wa kando na kuishia kuambukizwa maradhi ya zinaa. Hatimaye aliwambukiza mkewe, jambo analosema lilihatarisha ndoa yake.

Read ENGLISH VERSION

Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke ,kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdibn94gphmoZqlkZZ6orjIspypmaOqrm65z6KpmmWbnsGiusOapaJlp5a4osDIZq6aZZ2WwKmtzJuspaGqnnqiwMCkoLCZXaDCtq7Em5hmpaOWuaKuwGaumqOVY7W1ucs%3D