Mchanganuzi: Ruto anatumia ukabila katika kucheza siasa za Kibra

- DP Ruto anatumia kadi ya ukabila kwenye siasa za Kibra kulingana na mchanganuzi Manyora

- Ruto amekuwa akimsakia kura Mariga kupitia mikutano na wapiga kura kutoka Kibra

- Mariga anakabiliana na Imran Okoth wa ODM, Owalo wa ANC na wengine kwenye uchaguzi huo mdogo

Naibu Rais William Ruto amechomoa kadi ya ukabili na ndiyo anatumia kusakia mgombea wa Jubilee McDonald Raila kura kwenye uchaguzi mdogo wa Kibra, mchanganuzi wa kisiasa Herman Manyora amesema.

Manyora alimkosoa Ruto akisema taifa linafaa kukabiliana na ukabila na ni makosa kwa kiongozi yeyote kucheza siasa za ukabila.

Habari Nyingine: Matiang'i atangaza Alhamisi ni sikukuu ya umma

Manyora alidai DP amekuwa akikutana na jamii fulani kutoka Kibra nyumbani kwake Karen.

“Ni lazima tukabiliana na suala la ukabila, na pia huu ni uvunjaji wa sheria kwa mtu kutumia mali ya umma kuwashawishi wapiga kura. Nyumbani kwa Ruto Kareni ni kama tu Ikulu," alisema.

Mbunge wa Lang'ata Nixon Korir naye alipinga madai ya Manyora akisema hakuna kosa lolote katika DP kufanya mkutano na kundi la watu.

"Tuna makabila 42 Kenya na wakati ambapo jamii inajipanga na kukutana na DP, ni kinyume cha sheria? Hawa ni Wakenya ambao wanakutana ili kujadili mambo ya maendeleo," alisema.

Habari Nyingine: Matiang'i atangaza Alhamisi ni sikukuu ya umma

Jumanne, Oktoba 8, kulishuhudiwa rabsha kwenye lango la nyumbani kwa DP Ruto baada ya kundi la vijana waliofika hapo kukatazwa kuingia.

Duru ziliarifu kuwa mkutano uliokuwa ukiendelea ulikuwa wa wapiga kura wa Kibra kutoka jamii ya Abagusii.

Mbunge wa Mugirango Kusini Sylvanus Osoro alikiri kuwa wakazi wa Kibra kutoka jamii hiyo walikuwa wamekutana na Ruto.

“Kila aliyefaa kuhudhuria mkutano huo alitumiwa ujumbe kwa sababu tulipanga ziara hiyo kupitia makundi ya jamii yetu Wakisii. Walioalikwa walikuwa wameketi kwenye hema kufikia saa moja asubuhi na walikuwa watu 5,000 wa kabila letu wanaoishi Kibra,” Osoro aliambia gazeti la Nation la Jumatano, Oktoba 9.

Kinyang'anyiro kwenye uchaguzi huo mdogo utakaofanyika Novemba 7 ni kati ya Jubilee, ODM, ANC na wagombea wa kibinafsi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjZoVzhJhmpJygkaO0orrUs6BmqqWpvG6tzZqrrqWZlnq2t8CboKWZXaCutbXKmmSkrZOdsrutjKygmquRYseiecqimauZXp3Brrg%3D