Wakazi jijini Nairobi wameilimbikizia sifa chungu nzima kampuni ya magari ya uchukuzi ya Super Metro kwa huduma zake bora na kuwa na wafanyakazi wenye nidhamu
Habari Nyingine: Magazeti ya Jumanne, Februari 9: Mzee amcharaza mamake akitaka kumjua baba yake
Habari Nyingine: NTSA yafutilia mbali leseni ya Sacco ya Memba baada ya kifo cha abiria
Hii ni baada ya magari ya sacco hiyo kueneza kuhudumu zake katika barabara ya Ngong ambayo inatambulika kwa kuwa na msongamano mkubwa.
Hata hivyo, magari ya sacco zingine yamegoma yakipinga huduma za magari hayo kwenye barabara hiyo.
Inasemekana mamia ya abiria walikuwa wamekwama kwenye steji ya Ngong siku ya Jumatano, Februari 10 lakini Super Metro wakaingilia kati kuokoa hali livyokuwa.
Wanamitandao waliisifu kampuni hiyo na kuyataka magari yote ya uchukuzi kuiga mfano wa sacco hiyo.
Hapa baadhi ya maoni ;
"Magari ya sacco ya Supper Metro yana huduma bora zaidi kuliko magari mengine hapa jijini Nairobi na hata Kenya nzima, yana mpangilio na wafanyakazi wana nidhamu kwa abiria, " Kipkorir Anyeyo alisema.
" Kuna ukweli kuhusu magari ya kampuni ya uchukuzi ya Super Metro, ni miongoni mwa sacco ambazo zina huduma bora sana hapa Nairobi, hazina hitilafu za kiufundi na ni safi sana, hii sio sababu cartels hawayataki katika barabara hiyo," Road Alerts iliandika.
Haya yanajiri siku chache baada ya mwanamke mmoja kupoteza maisha yake akiwa ameabiri matatu moja ya sacco ya Memba.
Lucy Wanjiru anasemekana kutofautiana na utingo kuhusu kiwango cha nauli ambacho walikuwa wameafikiana alipe, katika harakati za kuzozana utingo alimrusha nje ya gari na kuondoka kwa kasi.
Wanjiru alifariki dunia Jumapili, Februari 7 baada ya kuachwa na majeraha mabaya kwenye kichwa chake.
Kwa sasa, huduma za magari ya sacco hiyo zimesitishwa kwa muda usiojulikana huku washukiwa wakisakwa na maafisa wa polisi.
Aidha, Shirika la NTSA limesema magari ya sacco hiyo yatafanyiwa ukaguzi upya na iwapo kutakuwepo na uvunjaji wa sheria, sacco hiyo itanyanganywa leseni.
Read: ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZX92g5BmpJqskanCbsXAZqqam5OkerqtjKysqZ2iYrqmwNGoZLOZpJa3uK2MpKywmV2jrm601J2sppldl7yzrYyymGato5azqr7IZ5%2BtpZw%3D