- Millicent Omanga anakashifiwa kwa kuchochea chaguzi ndogo za hivi punde za eneo bunge la Matungu na Kabuchai
- Omanga aliagizwa kufika mbele ya tume ya Uwiano na Utangamano NCIC kujibu madai hayo
- Hata hivyo Omanga alizua kizaa baada ya kucheleweshwa kuhojiwa kwa zaidi ya saa moja
Seneta Mteule wa chama cha Jubilee Millicent Omanga Jumatatu, Machi 8 alizua kizaazaa katika afisi za Tume ya Uwiano na Utangamano wa kitaifa, NCIC.
Habari Nyingine: Aliyekuwa Waziri wa Michezo Rashid Echesa afikishwa katika mahakama ya Kiambu

Habari Nyingine: Hatimaye Seneta wa Kakamega Cleophas Malala ajisalimisha polisi
Omanga alikuwa amefika katika afisi hizo kujibu madai kwamba alichochea katika chaguzi ndogo zilizofanyika katika eneo bunge la Matungu na Kabuchai.
Akiwa mwingi wa hasira, Omanga aliwakashifu maafisa wa tume ya NCIC kwa kuchukua muda wake mwingi ikizingatiwa alikuwa ahojiwa saa tano asubuhi lakini kufikia saa sita mchana hakuwa amehojiwa.
Wakati alipozua kizaazaa hicho, mbunge mwenzake wa Kasipul Charlse Were ndiye alikuwa bado anahojiwa na maafisa hao.
Kulingana na Omanga, tume hiyo ilimtaka afike afisini humo mwendo wa saa tano asubuhi lakini alighadhabishwa baada kusubiri kwa muda wa zaidi ya saa moja kuhojiwa.
Omanga alisema tume hiyo ingemuagiza afike mwendo wa saa sita badala ya saa tano, na pia kila aliyekuwa amehitajika kufika katika afisi hizo, angepewa muda na saa yake ili kuzuia kutatiza ratiba zao.
Habari Nyingine: Magazeti Jumatatu, Machi 8: Simu ya Rais Uhuru usiku yazima hasira ya Raila
" Tumesubiri hapa kwa zaidi ya muda wa saa moja, tutaendelea kusubiri kwa muda gani? Mngetuambia wakati sahihi ambao mnataka tuje, mimi ukiniambia saaa sita ningekuwepo wakati huo lakini mliniambia saa tano nimefika wakati huo lakini bado mnataka kuniweka hapa, kama mnajua kuhoji mbunge mmoja ingechukua zaidi ya saa moja basi mngefanya hesabu zenu ipasavyo,' Alisema Omanga.
Viongozi wengine ambao walitii amri ya kufika mbele ya tume hiyo ni mbunge wa Msabweni Feisal Bader, mbunge wa Mumias Mashariki Benjamin Washiali na mwenzao wa Kiminini ChrisWamalwa.
Wanasiasa hao wote wanakashifiwa kwa kuchochea ghasia katika chaguzi za hivi punde za eneo bunge la Matungu na Kabuchai.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZYJyfpNmqp6mlamubrnIpaOim5WjwW67zJqloJldlse2rYykoLOZka%2BuonnKmquio5Firqe10qJks5ldo7Cqr42hq6ak